Friday, July 7, 2017

TAARIFA YA UTENDAJI KAZI KATIKA SERIKALI YA WANACHUO (ARISO) MWAKA 2016/2017
Tunapenda kumshukuru Mungu wetu kwa wema na ulinzi wake tangu tulipokabidhiwa uongozi hadi leo tuko salaama, jina lake litukuzwe sana.
      Tulikabidhiwa uongizi rasmi tarehe 15/06/2016 na tukiwa  jumla ya wanachuo 171  

Malengo na madhumuni ya taarifa hii ni kujua mafanikio,malengo na changamoto katika serikali yetu ya ariso.

Chama cha ariso kilikuwa na malengo mbalimbali kama yalivyokuwa yanapendekezwa kwenye vikao na kwa kujinadi kipindi tunaomba kura kwenu kama ifuatavyo;


MALENGO
      I.            Kuinua uchumi wa ariso kwa kubuni miradi mbalimali.kama vile kuwa na jiko la kuchoma chipsi , kuwa na photocopy mashine kuwa na mashine ya kutengeneza vitambulisho itakayo kuwa ikitengeneza vitamburisho na vyeti katika chuo chetu na katika vyuo mbalimali na tasisi mbalimbali itakayo kuwa kama kitega uchumi wa ariso.
   II.            Kutengenza brogspot itakayo tumiwa na wanachuo na watu mbalimbali kupata tarifa za chuo.
III.            Kununua computer itakayotunza kumbukumbu za ariso kwa kila mwaka
IV.            Kusimamia matatizo yote ya wanachuo na kuhakikisha kila mwanachuo ameyafikia malengo yake kwa dhati .
  V.            Kusimamia ratiba ya masomo kuhakikisha kila darasa lina pata siku moja kwa kila wiki kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.
VI.            Kusimamia swala la maji, chakula pamojan na mazingira kwa ujumla
VII.            Kusimamia pesa na  mali za ariso  

MAFANIKIO;
Mafanikio yaliyopatikana tangu tupewe uongozi ni  mengi , kwa kuyataja kwa ufupi tu.
      I.            Tumefanikiwa kusimamia  matatizo na kero nyingi zinazotukabiri wanachuo kama vile ukosefu wan ndoo, mifagio ya vyumbani taa katika mabweni, taa madarasani, ubovu wa ofisi ya ARISO na mbao za kufundishia na kero zinginezo nyingi.
   II.            Tumefanikiwa kufungua blonspot inayoitwa  arisoardhi.blogspot ambayo ina email. Ariso.ardhi@gmai.com hii itatusaidia wanachuo  kupata habari mbali mabali katiaka chuo chetu.
III.            Tumefanikiwa kupeleka namba za simu za wanachuo na kusajiliwa na vifurushi vya university offer  tigo na voda
IV.            Tumefanikiwa kusimamia swala la ratiba na kuhakikisha kila darasa limepata siku moja kwa kila wiki kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo.
  V.            Tumefanikiwa kuanzisha mafunzo ya programs zinazoendana na masomo yetu tuliyoyaedesha kwa ratiba za usiku  hii imesaidia kujua program vizuri kwa kila mwanachuo kama vile Autocard na Arc GIS.
VI.            Tumefanikiwa kupewa week moja kwa ajili ya kujifunza practical kwa vifaa vya kisasa ikiwa kama study tua kwa wanafunzi.
VII.            Tumefanikiwa kusimamia swala la maji kwa kuhakikisha maji yanapatikana kwa kila mda na kuomba kuongezewa kwa tank za maji hapa chuoni.
VIII.            Tumefanikiwa kusimamia pesa ya ariso kwa kuhakikisha tumepewa kama pesa ya wanachuo
IX.            Tumefanikiwa na kusajiliwa kwa account yetu ya ARISO na BOT
  X.            Tumefanikiwa kufanya sherehe ya kuwakaribisha wanachuo wa mwaka wa kwanza.
XI.            Tumefanikiwa kusimamia DSTV na kuomba chuo watulipie kifurushi cha DSTV .
XII.            Tumefanikiwa kushirikiana na vyuo vingine katika sherehe mbalimbali kimawazo pamoja na michezo.
XIII.            Tumefanikiwa kununu vifaa vya michezo kama vile mipira
XIV.            Tumefanikiwa kupewa mipira miwili na watu wa LAPF na tumeomba jezi pia bado tunasubilia  .
XV.            Pia tumefanikiwa kujumuika na watu wa tigo wakatupa huduma zao na pia tukafanikiwa kuwaomba watuwezeshe vifaa vya michezo kama vile  jezi pamoja na mipira na pia wakakubari kuwashirikisha katika sherehe zozote pale tunapoandaa sherehe zetu kama vile welcome first year na graduation .

CHANGAMOTO
Zifutazo ni changamoto zilizo tukabiri katika utendaji kazi
      I.            Ukosefu wa mtaji utakao tuwezesha kuendesha miradi mbalimbali  itakayo kuwa kama kitega uchumi wa ariso.
   II.            Kutotekelezewa kero zetu mapema pale tunapo pata changamoto hapa chuoni .
III.            Ukosefu wa viwanja vya michezo hili limekuwa likitupa wakati mgumu sana pindi tunapohitaji mazoezi
IV.            Kutokuwa na bima kwa baadhi ya wanachuo hii imekuwa ikitupa wakati mgumu pale mwanachuo anapopatwa na tatizo kama vile kuumwa hadi inapelekea kwa viongozi kutumia pesa zao kutoka mifukoni mwao kumsaidia mwanachuo.
MAPENDEKEZO
·       Tunapendekeza uongozi utakao kuja uhakikishe kusimamia  kero bila kurudi nyuma
·       Mapendekezo yetu kuwa kwa wanachuo wote ambao hawana bima za afya ni ushauri kuwa kila mwanachuo awe na bima ya afya hii itamsaidia pale anapokuwa na tatizo lolote la kiafya .
·       Uongozi ujao usimamie swala la practical kwa kila darasa lipate hata siku moja kwa week.
·       Pia tunapendekeza viongozi watakaochaguliwa wasimamie kujifunza kwa programs na kuhakikisha kila mwanachuo anajua hizo software.
HITIMISHO
Shukrani za pekee kwa wanachama wote wa ariso  kwa ushirikiano wenu katika uongozi wetu muendele na moyo wa kusaidiana ili kuanda maisha yetu kwa pamoja na kuijenga ariso.

kwa niaba ya viongozi wenzangu tunasema asanteni sana Mungu awe pamoja nanyi awaongoze katika maandalizi ya mitihani na katika mitihani yetu.

0 comments :

Post a Comment