Tuesday, April 18, 2017

WIZARA YA ARDHI NYUMBA NA MAENDELEO  YA MAKAZI  CHUO CHA ARDHI MOROROGO
RISALA YA  WANAFUNZI WA  CHUO  CHA ARDHI MOROGORO KWA MGENI RASMI MAHAFALI YA 35 YA CHUO CHA ARDHI
TAR 24/03/2017
Ndugu mgeni rasimi,
Awali ya yote tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa kufika kwako hapa chuoni ,tunatambua kuwa umeacha shughuli zako nyingi za kiofisi na ukakubali kuchukua muda wako kuja kujumuika nasi katika shughuli ya kuwaanga ndugu zetu kwa pamoja tunasema asante sana Mungu awe pamoja nawe na karibu sana.
Ndugu mgeni rasimi;
Chuo hiki kiko chini ya  wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi na kilisajiliwa na Baraza la Taifa la elimu ya ufundi Tanzania (NACTE) tangu  tarehe 21/5/2002 na  chuo kinatumia mitaala ambayo ni “Competence based “ chuo kilipata  ithibati kamili (Full Accreditation) ya NACTE tangu mwaka 2010. Baada ya kutimiza vigezo vya elimu na mazingira ya uboreshaji elimu hiyo.


LENGO LA RISALA:
Ndugu Mgeni Rasmi,
Lengo la risala hii ni kukujulisha kuhusu mafanikio, changamoto, maoni na mapendekezo katika kuboresha hali ya kitaaluma na maisha mengine nje ya taaluma Chuoni hapa.

Ndugu mgeni rasimi; Chuo kinatoa kozi ya Jiomatikia katika ngazi zifuatazo:
Cheti cha awali cha Jiomatikia (Basic Certificate in Geomatics (NTA LEVEL 04)),
Astashahada ya Jiomatikia (Certificate in Geomatics (NTA LEVEL 05)),
Stashahada ya Jiomatikia (Diploma in Geomatics (NTA LEVEL 06)).
Ndugu mgeni rasimi:
Katika mahafali ya leo, kuna jumla ya wahitimu 171 kati yao wanafunzi wa jinsia ya kiume wakiwa ni 136 Na jinsia ya kike wakiwa  ni 35.
Ndugu mgeni rasimi;
Mafanikio yaliyopatikana tangu chuo chetu kianzishwe ni mengi , kwa kuyataja kwa ufupi tu ni kwamba kila mwaka chuo kimekuwa  kikizalisha wataalamu wazuri wenye kuleta ufanisi katika taaluma hii ya upimaji Aridhi, nchini ambao wameajiriwa katika Halmashauri mbalimbali na hivyo kuipunguzia serikali utegemezi wa wataalamu wa kigeni katika idara ya upimaji Ardhi.

CHANGAMOTO
Ndugu mgeni rasimi:
Malengo ya serikali ni utekelezaji wa sera ya upimaji ardhi kwa ajili ya mashirika na taasisi mbalimali, kutokana na ukosefu wa ajira wataalamu wengi hawanufaiki na taaluma inayotolewa katika chuo hiki hadi kupelekea wengi wetu kupoteza taaluma zetu kwa kukaa tu bila ajira. ndugu mgeni rasimi:
 kutokana na tatizo la ajira tunaamni wizara yako inao uwezo wa kupunguza au kuondoa kabisa tatizo hili kwa kutoa ajira pindi tunapomaliza muda wa mafunzo.
Ndugu mgeni rasimi:
Tunalo tatizo katika chuo chetu la kukosa vitendea kazi kwa ajili ya masomo yetu; Tunao Ukosefu wa maktaba (Library) kwani iliyopo bado haijaisha, jengo hili la maktaba limekuwa na muda mrefu tangu lifikie hatua hiyo, kwa sasa tuna  chumba kidogo cha kutunzia vitabu hivyo hali hii inatupa wakati mgumu wa kujisomea kwani tunakosa vitabu vya kutosha.
Ndugu mgeni rasimi;
 Tunao Ukosefu wa chumba cha computer (Computer Lab) kwani kilichopo ni kidogo chenye computer chache na baadhi ni mbovu hazitumiki, pia computer hizi hazina program za kitaaluma (software).
Ndugu mgeni rasimi;
Tunao Upungufu wa vifaa vya kujifunzia vinavyo endana na taaluma yetu kwani vilivyopo ni vichache, na vingine vimeshapitwa na wakati tunaomba tupatiwe vifaa za kisasa kama vile RTK GPS, na Differential GPS za kutosha ili tupate elimu inayoendana na wakati.
Ndugu mgeni rasimi;
Tunao Ukosefu wa vibweta vya kujisomea kwenye mazingira ya chuo, hivyo wanachuo kufanya majadiliano ya kimasomo (Group Discussion) kwenye mazingira magumu,
Ndugu mgeni rasimi;
Serikali kupitia wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya makazi  ilikuwa ikitupatia  stationary Allowance Tsh 50,000 /= kila mwanachuo,  pesa hii ilikuwa inasaidia kumudu gharama zote za stationary kwa wanachuo lakini mwaka wa masomo 2016/2017 hatujapewa hii imepelekea kwa mwanchuo kuto mudu gharama za stationary.
Ndugu mgeni Rasimi;
 ombi letu kuwa serikari kupitia wizara ya Ardhi Nyuma na Maendeleo ya makazi ituhudumie stationary allowance kwa kila mwanafunzi kwa kila mwaka kama ilivyokuwa hapo awali, pia tunaomba mchakato wa kutoa mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya kati uharakishe ili kupunguza ugumu wa kugharamia elimu wazazi wetu.
Ndugu mgeni rasim;
Miundombinu mingi imechakaa na ina tufanya tuishi katika mazingra magumu; Uchakavu wa madarasa (madirisha, feni na mifumo ya umeme kusababisha hitilafu kila mara madarasani). Mabweni yaliyopo yamechakaa sana, sakafu, paa, kuta, madirisha, na milango vimechakaa sana kiasi cha kutokuwa rafiki kwa wanachuo na hayatoshi. Hivyo kupelekea kukaa wanafunzi wastani wa sita mpaka nane chumba kimoja. Uchakavu wa vyoo vyote vinavyo patikana hapa chuoni kwani vingi havijafanyiwa ukarabati vinaziba mara kwa mara na kusabisha usumbufu kwa wanachuo.
Ndugu mgeni rasimi;
Chuo hakina viwanja vya michezo, hii inatupa wakati mgumu tunapohitaji mazoezi nakupelekea kushindwa kuendesha michezo hapa  chuoni. Tunaomba uwezeshwaji kutoka wizara yako wa kujenga eneo la chuo lililopo mlima kola. Tunao upungufu wa tank za kutunzia maji, hii imepelekea kutokuwa na uhakika wa maji hapa chuoni kwani tank iliyopo ni ndogo na halikidhi mahitaji.




Ndugu mgeni rasimi;
tunakutakia kila la kheri katika kazi zako za ujenzi wa Taifa na tunatumaini na kuamini  kuwa matatatizo tuliyowasilisha kwako katika risala hii yatapatiwa ufumbuzi wa kudumu. Nasi kwa pamoja tunashukuru sana kwa kuweza kuonesha moyo wa upendo, kujali na kuvumilia yote na kuweza kufika hapa chuoni isiwe kikomo chako cha kututembelea mara kwa mara kujua maendeleo ya chuo chetu na mapungufu yatakayojitokeza katika chuo chetu tukiwa kama wanafamilia wa wizara yako Mungu awe pamoja nawe .

Risala hii imeandaliwa na Mwenyekiti wa serikali ya wanafunzi wa chuo cha Ardhi Morogoro
NDG. MAGOMBA  PETER  MAHOTA- RAIS ARISO

………….Ahsante sana…………..



0 comments :

Post a Comment